Burudani
Karrueche Tran apuuzia kilio cha Chris Brown kwenye remix ya Back To Sleep
Karrueche Tran hayupo tayari kumrejesha Chris Brown kwenye maisha yake licha ya muimbaji huyo kumuomba warudiane kwenye remix ya wimbo wake “Sex You Back To Sleep,” kwa mujibu wa ripoti mpya.
Chris na Karrueche waliachana March mwaka jana baada ya staa huyo kuzaa na model, Nia Guzman. Mtandao wa Urban Islandz uliripoti kupitia vyanzo kuwa Brown aliwasiliana na mrembo huyo baada ya kuachia wimbo huo lakini alimpuuzia.
Hadi sasa msichana huyo hajajibu chochote tangu wimbo huo walioshirikishwa Zayn Malik na Usher utoke. Chris amelitaja jina la Karrueche kwenye wimbo huo.