Habari
Janeth Jackson na mumewe wana mpango wa kuasili mtoto Syria ama Jordan
Yalianza mapenzi, ikafuata ndoa, na sasa anatafutwa mtoto ili kuikamilisha familia yao mpya mwimbaji Janeth Jackson na mumewe mfanyabiashara billionea Wissam Al Mana wa Qatar.
Kwa mujibu wa US Weekly chanzo kimoja kimethibitisha kuwa Janeth (47) anafanya utafiti wa kimya kimya juu ya taratibu wa kuasili mtoto kutoka nchi ya dunia ya tatu.
Habari zaidi zinasema kuwa pop star huyo amemfuata Queen Rania wa Jordan ili amsaidie kumuwezesha kuasili mtoto.
Janeth Jackson ambaye ni mke wa Wissam Al Mana walianza uhusiano (2010 na baadaye kufunga ndoa. Al Mana ni mume wa tatu kwa Janeth ambaye hapo kabla alikuwa ameshaolewa mara mbili.