Michezo

John Bocco yupo tayari kuikabili El Masry

Afisa habari wa klabu ya Simba, Haji Manara amesema kuwa hali ya mshambuliaji wao, John Bocco inaendelea vizuri na huwenda akacheza endapo kocha atampatia nafasi hiyo.

Manara ameyasema hayo wakati akijibu maswali ya baadhi ya mashabiki wa timu hiyo waliyotaka kufahamu hali ya mchezaji huyo kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram.

Niwajuze tu kuwa hali ya Bocco anaendelea vizuri na yupo tayari kucheza kama kocha atampanga.

Miongoni mwa wachezaji wa kikosi hicho cha msimbazi wanao tarajiwa kurejea hivi punde ni pamoja na mlinda mlango bora wa michuano ya COSAFA  2017, Said Nduda.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents