Michezo

Kabla kutua Dar kikosi cha Simba SC chakutana na Balozi wa Tanzania nchini Misri

Viongozi wa klabu ya Simba wakiongozwa na Rais Salim Abdallah pamoja na wachezaji wao hapo jana wamepata nafasi ya kualikwa na Balozi wa Tanzania nchini Misri Balozi Gen Issa Nassor nyumbani kwake kabla ya kuanza safari ya kurejea nchini Tanzania.

Mnyama Simba SC atolewa kiume na Waarabu wa Misri

Simba inatarajia kurejea nchini mapema hii leo ikitokea nchini Misri ilipokuwa ikicheza mchezo wake wa kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya timu ya Al Masry.

Katika mchezo huo Simba SC ilitoka sare ya bila kufungana na kuyaaga mashindano hayo baada ya mchezo wake wa awali uliyopigwa jijini Dar es Salaam kutoka sare ya mabao 2 – 2.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents