Kelly Rowland atumbuiza kwenye ‘private party’ katika jumba la kifahari la bilionea wa Afrika Kusini
Haijalishi iwe ni Kipaimara, vigodoro au birthday, kama mkwanja upo basi unaweza kumleta staa yeyote kutumbuiza. Baada ya rapper Kanye West kutumbuiza katika harusi ya mjukuu wa Rais wa Kazakhstan hivi karibuni, staa mwingine wa Marekani Kelly Rowland atumbuiza katika jumba la bilionea wa Afrika.
Mwimbaji wa R&B na member wa zamani wa kundi la Destiny’s Child mwishoni mwa mwezi uliopita (September) alikuwa nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kutumbuiza katika ‘private party’ kwenye jumba la kifahari ‘mansion’ la Bilionea Douw Steyn.
Hii ndio mansion ya Steyn iliyoko Afrika Kusini ambapo Kelly alienda kutumbuiza
Rowland aliwasili nchini humo Sept 25 kwaajili ya kupamba ‘private party’ ya siku mbili Sept 27 na 29 mwaka huu katika jumba hilo ambalo limeanza kujengwa toka (2008) mpaka kukamilika kwake.
Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela anayedaiwa kuwa rafiki mkubwa wa billionea huyo alitarajiwa kuwa mmoja wa wageni maalum katika party hiyo ya siri iliyopangwa kuhudhuriwa na wageni wa VIP.
Bilionea Douw Steyn wa Afrika Kusini
Akiwa na utajiri unaokisiwa kuwa Rand bilion 8, Steyn ni mmiliki wa Hotel ya Lavish Saxon iliyoko Joburg na mwanzilishi wa makampuni ya Auto and General and Budget Insurance Company.
Kazi na dawa! Akiwa Afrika Kusini Kelly Rowland alitweet picha akiwa anakula good time na Simba mtoto na kuelezea jinsi alivyotaka kumdhuru.
RAWRRRR! *In my Blue voice* I held a baby lion in South Africa!!! Until he almost took my shoulder off… http://t.co/dhme6ibNlX
— KELENDRIA ROWLAND (@KELLYROWLAND) October 3, 2013
SOURCE: SOWETAN