Michezo
Kikosi cha Uingereza chapewa mbinu za Kihindi kuelekea kombe la Dunia Urusi
Kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza kimeendelea na mazoe yake chini ya kocha, Gareth Southgate kuelekea michuano ya kombe la Dunia inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi mwezi huu nchini Urusi.
Uingereza inajaribu kutumia kila njia ya mafunzo ili kuhakikisha inakiweka sawa kikosi chake kama baadhi ya wachezaji walivyooneka wakitumia mchezo maarufu wa India ujulikanao kwajina la ‘Kabaddi’ kama sehemu yao ya mazoezi.
Wachezaji wenye majina makubwa kama, Harry Kane, Dele Alli na Marcus Rashfod ni sehemu ya waliyofanya mazoezi hayo kwa mfumo wa makundi.
Kocha wa timu hiyo, Southgate anahaha kuhakikisha wachezaji wake wanakuwa makini na mashindano hayo na kufanya kazi kwa pamoja.
Mchezo wa Kabbadi ukiwa unachezwa na wahindi