Michezo
Kiungo wa Tusker FC, Abdul Hillary Hassan atua klabu ya KMC
Klabu ya KMC imefanikiwa kumsajili kiungo, Abdul Hillary Hassan kwa kandarasi ya mwaka mmoja akitokea nchini Kenya.
Hillary Hassan ni kiungo mshambuliaji raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 23 na kupata bahati ya kuchezea klabu ya African Lyon msimu wa mwaka 2014-16 kabla ya kutimkia Kenya mwaka 2017.
Akiwa nchini Kenya, Abdul Hillary Hassan amechezea klabu ya Tusker fc inayoshiriki ligi kuu na kupata nafasi ya kuitwa kwenye timu ya taifa Kilimanjaro Stars na kushiriki michuano ya CECAFA Senior challenge cup 2017.