Michezo
Kombe la dunia la Klabu: Sanfrecce Hiroshima ya Japan yazima matumaini ya TP Mazembe
Matumaini ya TP Mazembe kufika kwenye fainali za kombe la dunia la klabu yamezimwa jana baada ya mabingwa hao wa Afrika kufungwa mabao 3-0 na Sanfrecce Hiroshima ya Japan.
Mchezo huo ulipigwa kwenye uwanja wa Yanmar wa mjini Osaka, Japan.
Magoli hayo yalifungwa na Tsukasa Shiotani, Kazuhiko Chiba na Takuma Asano.
Kikosi cha Mazembe kilikuwa kikiundwa na wachezaji wa kimataifa kutoka Ivory Coast, Mali, Zambia, Tanzania, Ghana na mchezaji mmoja tu kutoka DR Congo.
Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatta nao walishindwa kutamba baada ya nafasi ya pekee walizopata kushindwa kuzitumia vyema.
Sanfrecce Hiroshima itakutana na River Plate ya Argentina kwenye nusu fainali December 16 huku Barcelona ikikutana na Guangzhou Evergrande December 17.