Michezo
LeBron James atimka Cleveland Cavaliers aingia kandarasi ya miaka minne klabu hii
Mchezaji wa mpira wa kikapu nchini Marekani, LeBron James ameingia kandarasi ya miaka minne ya kuitumikia Los Angeles Lakers na kuachana na klabu yake ya Cleveland Cavaliers aliyoanza kuitumikia tangu mwaka 2014.
Wakala wa James amezungumza na vyombo vya habari hapo jana siku ya Jumapili na kusema kuwa wamekubali dili hilo la miaka minne lenye tahamani ya fedha dola za Kimarekani milioni 154 sawa na pauni milioni 117.
Hii ni kwa mara ya pili kwa mchezaji huyo kuachana na klabu yake ya Cleveland Cavaliers inayoshiriki ligi ya NBA baada ya kufanya hivyo mwaka 2010 alipo timkia Miami Heat na kurejea mwaka 2014.