Michezo

Leicester wanaukaribia ubingwa wa EPL baada ya kuifunga Newcastle

Klabu ya Leicester City wamezidi kukaa kileleni mwa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kupata ushindi dhidi ya Newcastle.

160314205249_shinji_okazaki_640x360_afp_nocredit

Lecester waliiifunga Newcastle, waliokuwa wakicheza mechi yao ya kwanza chini ya meneja mpya Rafael Benitez, kwa bao 1-0 mechi hiyo iliyochezwa Jumatatu usiku.

160315045917_shinjiokazakioverheadkickgetty

Shinji Okazaki ndiye aliyewafungia bao hilo la pekee, na alilifunga kwa ustadi wa aina yake dakika ya 25.

Leicester City sasa wanazidi kukaribia kushinda taji lao la kwanza kabisa la ligi zikiwa zimesalia mechi nane msimu huu.

Newcastle walionekana kuimarika na walikaribia kufunga kupitia Ayoze Perez na Moussa Sissoko lakini bahati yao haikuwa yao.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents