Michezo
Liverpool yakamilisha usajili wa Christian Benteke
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mshambuliaji kutoka nchini Ubelgiji, Christian Benteke Liolo mwenye umri wa miaka 24, kwa ada ya usajili wa pound milioni 32.5 akitokea Aston Villa.
Benteke amejiunga na Liverpool kumaliza utata na ukame wa magoli katika safu ya ushambuliaji huko Anfield, baada ya kuondoka kwa Raheem Sterling aliyetimkia Manchester City mwanzoni mwa juma hili.
Benteke aliifungia Aston Villa mabao 13 katika michezo 26 ya ligi kuu ya soka nchini England aliyocheza msimu uliopita na alikua sehemu ya kikosi kilichoifikisha kwenye hatua ya fainali ya kombe la FA The Villian kabla ya kufungwa na Arsenal katika fainali.