Mitindo
Martin Kadinda kuonyesha ‘Ushababi’ wa Wanaume wa Dar katika maonyesha ya mavazi Lagos (Audio)
Mbunifu wa Mavazi ya Kiume na mshindi wa tuzo mbalimbali za mavazi Afrika Mashariki, anatarajiwa kuzindua collection yake mpya ya Mavazi Jijini Lagos nchini Nigeria Weekend hii.
Kadinda muda mfupi akiwa Uwanja wa ndege wa kimataifa amezungumza na Bongo5 na kushukuru watanzania kwa support wanayotoa katika sanaa Ya ubunifu, pia ameishukuru Basata kwa kuwa msaada mkubwa katika kupata vibali kwa vyote kumuwezesha kusafiri.
Pia Kadinda ameonyesha kufurahishwa na serikali ya Jamuhuri katika kuweka utaratibu mzuri kwa wasanii kuweza kuweza kutangaza nchi kupitia fani ya Ubunifu.
Mbunifu huyo atakuwa nchi Nigeria katika week ya maonyesho ya mavazi ya Kiume na pia atashiriki katika utoaji wa tuzo Kubwa za mavazi zinatambulika kwa jina la Man awards.