Habari
Mbunge wa Chadema ajiuzulu na kujiunga na CCM
Mbunge wa Jimbo la Serengeti mkoani Mara, Marwa Ryoba Chacha amejiuzulu Ubunge wa jimbo hilo muda huu akieleza ni katika kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli.
Kwa mujiubu wa Azam tv, Akizungumza hapo jana Septemba 27 Marwa amesema amechukua uwamuzi huo kumuunga mkono mwenyekiti wa CCM, Rais Magufuli.
Amesema wakati akigombea ubunge aliahidi kuwaletea maendeleo wananchi wake lakini dhamira yake haijafanikiwa kutokana na vikwazo anavyokumbana navyo ndani ya Chadema.