Mchizi Wangu (Remix)
Imekuwa ni historia katika gemu la muziki wa kizazi kipya hapa nchini kwa kuwepo kwa ugumu wa kuwakutanisha wasanii wenye uwezo mkubwa kisanaa na kuwafanyisha wimbo wa pamoja, lakini la kufurahisha hivi karibuni kwa mara ya kwanza wakali kibao wa muziki wa Hip Hop wameunganika na kufanya mkono wa pamoja..
Imekuwa ni historia katika gemu la muziki wa kizazi kipya hapa nchini kwa kuwepo kwa ugumu wa kuwakutanisha wasanii wenye uwezo mkubwa kisanaa na kuwafanyisha wimbo wa pamoja, lakini la kufurahisha hivi karibuni kwa mara ya kwanza wakali kibao wa muziki wa Hip Hop wameunganika na kufanya mkono wa pamoja ambao umeonekana kuwa bora kabisa kuliko ngoma zote za ushirikiano zilizowahi kufanyika.
Wimbo wa wasanii Nako 2 Nako We ndo mchizi wangu hivi karibuni umerudiwa na kufanyiwa remix ambayo imewakutanisha wasanii kibao na wakali akiwemo, Jay Moe, Fid Q, Mansu-Li, Geez Mabovu, Dr K wa Mapacha, Adili Chapakazi, Chidi Benz, Mwanafalsafah, Mheshimiwa Temba, Babuu wa Kingoko na wenye ngoma yao ambao ni Nako 2 Nako Souldierz.
Bongo5 ilipata fulsa ya kuisikiliza ngoma hiyo ambayo imerudiwa katika studio za MJ Records na Prodyuza Marco Charlie, dah ukweli kila mtu amefanya vizuri lakini wapo baadhi ya wasanii ambao wanaonekana kuhemea mipira ikiwa na maana wamejitahidi kufanya kile walichoweza japokuwa wameonekana kumezwa na baadhi yao.