Michezo

Michael Carrick atangaza kutundika daluga Manchester United

Kiungo wa Manchester United, Michael Carrick ametangaza rasmi kustaafu soka mwishoni mwa msimu huu.

Carrick mwenye umri wa miaka 36, amecheza jumla ya michezo  463 ndani ya United toka ajiunge akitokea Tottenham kwa pauni milioni 18 mwaka 2006 na kufanikiwa kushinda mataji 34 nchini Uingereza.

Kiungo huyo amesema kuwa unafika muda mwili wako unakuambia ‘stop’, na hivyo ndivyo ilivyo kwangu kwa sasa.

Mwezi Januari meneja wa timu hiyo, Jose Mourinho  amesikika akisema kuwa angelijiskia furaha endapo Carrick ataamua kusalia ndani ya  klabu

 

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents