Burudani

Mimi Mars aeleza kwanini Vanessa alizushiwa kuwa mjamzito

Msanii Mimi Mars amefunguka sababu ya Vanessa Mdee kuzushiwa kuwa ni mjamzito.

Muimbaji huyo ambaye ni ndugu na Vanessa Mdee ameiambia Funiko Base ya Radio Five kuwa ulaji wa Vanessa ni miongoni mwa vitu vilivyopelea watu kuhisi hivyo.

“Hapana haiwezi kutokea, namuona kila siku ni kwamba anakula sana, mahaba ni mengi kwa hiyo wanafurahia lakini hakuna kabisa (mimba),” amesema Mimi Mars.

Vanessa Mdee yupo katika mahusiano na muimbaji mwenzie, Jux.

Licha ya kufanya vizuri katika muziki na kutokea familia moja, Vanessa na Mimi Mars hawajawahi kutoa wimbo wa pamoja zaidi ya kushirikishwa na ndugu yao mwingine anayefanya muziki wa Injili, Nancy Hebron katika wimbo uitwao Beautiful Jesus.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents