‘Mission’ ya Juventus kumnasa meneja wa Chelsea, Maurizio Sarri baada ya fainali ya Europa League hii hapa, muda pekee ndiyo unao subiriwa
Kocha asiye na maneno mengi ndani ya ligi kuu England na mpenzi mkubwa wa kutumia sigara kama sehemu ya kiburudisho chake, Maurizio Sarri ameendelea kuwa chaguo kubwa la vibibi vya turin klabu ya Juventus huku miamba hiyo ya soka ya Italia ikitarajia kumpatia kandarasi mara baada ya fainali za Europa League.
Sarri kwa sasa anakiandaa kikosi chake kuikabili Arsenal huko Baku kunako Mei 29 huku akiwa hana uhakika na maisha yake ndani Stamford Bridge licha ya kuiweka The Blues katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi hiyo na kuwa kwenye uwezekano wa kutwaa taji kubwa la Europa League.
Mbele ya gazeti la michezo la Gazzetta dello Sport lililotoka hii leo siku ya Ijumaa limemuhusisha kocha huyo wa Chelsea na Juventus
Ukiachia mbali Sarri, klabu ya Juventus pia imeonyesha nia ya yakumtaka kocha wa Tottenham, Mauricio Pochettino lakini mipango hiyo inaonekana kuwa migumu kutokana na Muargenta huyo kuwa na kandarasi na timu hiyo ya London Kaskazini.
Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola pia amehusishwa lakini Sarri ameonekana kuwa ndiyo tageti kubwa ya miamba hiyo ya soka kutoka Italia.
Bosi huyo wa zamani wa Napoli, ametokea kwenye kurasa za mbele za gazeti la michezo la Ijuma hii La Gazzetta dello Sport kutoka Italia na kuripotiwa kuwa Sarri alikuwa kwenye kikao cha siri na Mkurugenzi wa timu ya Juventus, Fabio Paratici.
Hata hivyo, Paratici alifanya ziara yake hadi jijini London kukutana na kaka wa kocha wa Spurs, Pochettino ambaye inadaiwa kuwa ndiye wakala wake ambao wote hawa wanatazamiwa kuchukua mikoba ya Allegri.
Sarri anawavutia Juventus kutokana na uwajibikaji wake kwa maendeleo ya wachezaji na aina ya mfumo wake wa uchezaji.