MMC: ‘Siri ya Mchezo’ ya Fid Q yaingia, Diamond amuondoa Ommy Dimpoz na kukaa kileleni katika Marimba Music Chart (7th Nov 2013)
Wiki hii katika chart rasmi ya muziki wa kizazi kipya Tanzania ‘MMC’, wimbo mpya wa Fareed Kubanda aka Fid Q aliyomshirikisha Juma Nature ‘Siri ya Mchezo’ umeingia kama ingizo jipya, huku Diamond Platnumz akifanikiwa kumuengua Ommy Dimpoz kileleni na kukamata nafasi ya kwanza.
Yapo mabadiliko kadhaa katika chart ya wiki hii, nyimbo nne zimeingia na nyimbo nne zimeiaga Marimba Music Chart huku baadhi ya nyimbo zilizoendelea kuwepo zikiwa zimebadilishana nafasi.
Marimba Music Chart (MMC) ni chart rasmi ya muziki wa kizazi kipya Tanzania, ambayo huandaliwa na BONGO 5 kila wiki kutokana na Chart za Radio mbalimbali (zinazowakilisha radio zote) Tanzania.
HII NDIO CHART RASMI YA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA TANZANIA WIKI HII (7th November 2013)
Ingia HAPA kupata chart ya Marimba ya wiki iliyopita (01st November 2013)
VYANZO:
VIGEZO:
MMC inatumia Chart za radio mbalimbali za Tanzania (sample) kuchuja na kupata orodha ya nyimbo zilizoingia katika chart nyingi zaidi na kupata nyimbo 20 ambazo ndio zinazofikia kigezo cha kuingia katika Marimba Music Chart.