Michezo

Mourinho awalinganisha Barcelona na watoto wadogo U14, baada ya kipigo dhidi ya Liverpool ‘Watoto wamelala/ ni kitu kigumu kwangu kuelezea’

Aliyekuwa kocha wa klabu ya Real Madrid, Jose Mourinho amesema kuwa anashindwa kuamini kwa matokeo waliyopata Barcelona dhidi Liverpool kwenye mchezo wa nusu fainali ya Champions League uliyopigwa usiku wa hapo jana kwenye uwanja wa Anfield.
Kupitia mahojiano yake na chombo cha habari cha beINSPORT, Mourinho amewalinganisha Barcelona na watoto wa dogo wa liyo na umri chini ya miaka 14.

“Kama unaangalia bao lile kwa watoto wa chini ya umri wa miaka 14 au 15 ungeweza kusema, watoto wamelala, watoto hawapo sawa kiakili kucheza mpira, watoto wanahitaji kujifunza zaidi kuhusiana na msingi wa mechi.”  Mourinho ameiyambia beIN SPORTS.

Jose Mourinho ameongeza “Lakini tunazungumzia wachezaji bora kabisa ulimwenguni, bao ambalo hukuonyesha kwamba hakukuwa sawa kiakili.”

“Katika kipindi cha mapumziko nilisema kama Liverpool watafunga bao la pili basi hali ya uwanja itabadilika, na hakika yakibadilika yatakuwa mazingira magumu sana kwenda nayo sawa.”

“Lakini Barcelona wanabaadhi ya wachezaji bora kabisa ulimwenguni. wenyewe asili yao ni kucheza levo ile ile. asili yao kucheza dhidi ya Real Madrid, kuingia fainali, nusu fainali ya  Champions League final kila msimu kwao ni kitu cha kawaida.”

“Ni kitu kigumu sana kwangu kukielezea, ni vigumu sana kuamini kwamba timu yangu imeshinda mabao 3-0 kwenye mchezo wa kwanza alafu nakuja kupoteza 4-0 mechi ya marudiano. Ningelipenda kuona Valverde akijaribu kuelezea lakini naamini itamuwia ugumu kwake kuzungumzia.”

Kwa matokeo hayo ya jumla ya mabao 4 – 3, Liverpool sasa inasubiria mshindi kati ya timu ya Ajax au Tottenham ili kucheza kwenye hatua ya fainali ya michuano hiyo mikubwa barani Ulaya.

Mourinho amewahi kuikabili mara kadhaa Barca wakati akiwa kocha Mkuu wa Real Madrid mwaka 2010 hadi 2013.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents