Burudani
Mtanzania Emanuel Austin achagua wanafunzi 30 kwenye mashindano ya dansi Ujerumani
Emanuel Austin ambaye ni mwalimu wa dansi nchini Ujerumani, amefanya uchaguzi wa wanafunzi ambao watashiriki katika mashindano ya mwakani.
Akiongea na Bongo5, Austin ambaye amekuwa Balozi mkubwa wa muziki wa Tanzania nchini humo amesema, amechagua wanafunzi 30 ambao ndio watashiriki katika mashindano ya kudansi kuanzia mwezi April mpaka Julai mwakani.
Mwalimu huyo ameongeza kuwa katika kuchagua wanafunzi hao aliwaalika walimu wengie wa dansi ambao nao walikuwa kama majaji.