Burudani
Octopizzo awajibu wabaya wake wanaomuandama kwa maneno ya kashfa
Rapper wa Kenya, Octopizzo amefunguka kwa kuwajibu wabaya wake wanaomtupia maneno mabaya kwa kusema kitendo hicho kinaonyesha ni jinsi alivyo mkubwa zaidi.
Msanii huyo amekiambia kipindi cha Friday Night Live cha EATV, “Mimi ni sawa na big fish, when u are a big guy, everyone wants a piece of you, unajua mti wenye matunda ndio unapigwa mawe, so i’m a big fish.”
Octopizzo ameongeza kuwa atafanya kazi na rapper Khaligraph Jones endapo atalipwa kwa ajili ya kazi hiyo nje ya hapo haitawezekana.
Kwa sasa rapper huyo yupo nchini kwa ajili ya ziara yake kwenye vyombo vya habari.