MichezoUncategorized

Picha: Hatua iliyofikia uwanja wa White Hart Lane wa Tottenham

Mambo yanazidi kwenda vizuri katika uwanja wa Tottenham Hotspurs, White Hart Lane ambao unafanyiwa marekebisho ya upanuzi ili uweze kuchukua mashabiki wengi zaidi.

Uwanja huo ambao ulifunguliwa kwa mara ya kwanza 4 September 1899 ulikuwa na uwezo wa kuchukuwa watazamaji 36,284 lakini baada ya matengenezo hayo kukamilika utakuwa na uwezo wa kuchukuwa watazamaji 62,000 kwa mara moja.

White Hart Lane umefungwa Mei 14 mwaka 2017 na kuanza kufanyiwa marekebisho hayo ambayo yatagharimu kiasi cha paundi milioni 750. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa timu hiyo Daniel Levy amesema uwanja huo utaanza kutumika kwenye msimu wa August 2018/19.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents