Picha
Picha: Kajala ajichora tattoo ya jina la Wema
Katika kile kinachoonekana kama kuonesha shukrani zake za dhati kwa Wema Sepetu kutokana na kumtolea shilingi milioni 13 za hukumu yake siku kadhaa zilizopita, muigizaji wa filamu Kajala Masanja amejichora tattoo ya jina la Wema.
Wema ameiweka picha hiyo kwenye akaunti yake ya Instagram na kuandika, “ Me corazon…. she calls me her hero…. I sooo much appreciate her… my friend, my sister.. I’m happy… #pureheart….. nothing but a pure heart.”
Kajala alihukumiwa kifungo cha miaka 5 mitano jela au faini ya shilingi milioni 13 zilizotolewa na Wema. Pia Wema ameshare picha za tattoo zake mpya za kichina.