Michezo

Picha: Maelfu ya watu wajitokeza kumuaga mchezaji wa Fiorentina Italia

Maelfu ya watu wamejitokeza katika eneo la kanisa la Santa Croce church, Florence kuaga mwili wa marehemu Davide Astori ambaye alikuwa mchezaji na kepteni wa Fiorentina.

Astori alifariki katika chumba cha hotel Jumapili iliyopita masaa machache kabla ya timu yake kujitupa uwanjani kucheza mchezo wa ligi kuu Italia.

Miongoni mwa watu waliohudhuria ni kikosi cha wachezaji wa Fiorentina, wachezaji wa Juventus ambao usiku wa jana walikuwa London kucheza na Tottenham Hotspurs katika mchezo wa UEFA, kocha wa Inter Milan Luciano Spalletti, Mario Balotelli, Filippo Inzaghi na wengine.


Kikosi cha wachezaji wa Fiorentina

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents