Picha
Picha: Mwanamuziki wa Marekani Maya Azucena atumbuiza jijini Dar es Salaam
Ubalozi wa Marekani jana usiku uliandaa show maalum kuadhimisha siku ya wanawake duniani ambapo msanii wa Marekani Maya Azucena alitumbuiza akisindikizwa na wasanii wa Tanzania akiwemo Linah na wengine. Show hiyo iliyohudhuriwa na raia wengi wa kigeni ilifanyika kwenye kiota cha burudani cha Triniti kilichopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Show hiyo iliratibiwa na kampuni ya Megaparties Entertainment na kudhaminiwa na ubalozi wa Marekani.
Pamoja na kuwa mwanamuziki, Maya Azucena ni mwanaharakati wa haki za wanawake na ameshatumbuiza katika nchi kadhaa duniani kupromote uwezeshwaji kwa wanawake na wasichana na kukuza uelewa kuhusu ukatili wa kijinsia.
Bongo5 ilikuwepo kwenye burudani hiyo na hizi ni baadhi ya picha.