Michezo
Picha: Real Madrid wakwea pipa kuifuata Bayern Munich
Kikosi cha Real Madrid kikiwa na nyota wake Cristiano Ronaldo kimekwea pipa hii leo siku Jumanne kuelekea Munich kwaajili ya mchezo wake wa klabu bingwa barani Ulaya.
Vijana hao wa Zinedine Zidane watawakabili Bayern Munich kwenye mchezo wa nusu fainali ya klabu bingwa barani Ulaya unaotarajiwa kupigwa hapo kesho siku ya Jumatano.
Ronaldo akiwaongoza wachezaji wenzake wameonekana wakiwa wamevalia ‘suite’ nyakati za asubuhi wakielekea ndani ya ndege tayari kutua Ujerumani.
Zinedine Zidane akiwa na kikosi cha wachezaji 24 wameelekea Allianz Arena wakiwa sambamba na rais wao, Florentino Perez.
Wakati Real Madrid ikikwea pipa, wapinzani wao timu ya Bayern Munich asubuhi ya leo imekuwa bize na mazoezi.