Picha
Picha: Safari ya Kala Jeremiah kuelekea Morogoro kukabidhi tuzo yake kwa mama yake Mangwair
Mshindi wa tuzo tatu za KTMA 2013, Kala Jeremiah, leo ameelekea mjini Morogoro kwenda kuikabidhi tuzo yake msanii bora wa Hip Hop kama alivyoahidi: Kala Jeremiah atangaza kumpata marehemu Ngwair tuzo ya msanii bora wa Hip Hop, ataipeleka Morogoro.
Kala akiwa ameshika tuzo anayokwenda kumkabidhi mama yake Mangwair
Hizi ni baadhi ya picha hizo. Mwandishi wetu Yasin Ngitu yupo pamoja kwenye msafara huo unaongozwa na Kala, washkaji zake na waandishi wengine wa habari.