Picha

Picha: Wasanii waungana na Mstahiki Meya wa Ilala, Jerry Slaa kwenye kampeni ya uchangishaji madawati

Wasanii wa sanaa za uchoraji nchini, wameungana na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Slaa kwenye kampeni yake ya kila mwaka (Mayor’s Ball) kuchangisha madawati kwaajili ya shule za manispaa hiyo.

IMG_9076
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Slaa akiongea na waandishi wa habari leo kwenye hoteli ya Hyatt Regency Kilimanjaro jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni mchoraji Robino Ntila

Ili kusaidia uchangishaji wa fedha hizo Hyatt Regency Kilimanjaro Hotel itaendesha mnada wa hisani ambapo fedha zitakazopatikana zitatumika kununua madawati. Akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari, mstahiki meya huyo aliishukuru Hyatt Regency kwa msaada wake wa kudhamini shughuli hiyo ambapo jumla ya wasanii 10 watakaa kwenye hoteli hiyo kwa siku tano na kuchora picha mbalimbali zitakazopigwa mnada kwaajili ya kampeni hiyo.

IMG_9070
Mkurugenzi Mkuu wa Hyatt Regency Kilimanjaro Hotel, Trevor Saldanha

IMG_9088
Trevor Saldanha akiongea na waandishi wa habari

Picha hizo zitauzwa kwa wageni waalikwa watakaohudhuria mnada huo wa hisani utakaofanyika November 16.

IMG_9074
Mstahiki Meya Slaa akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari leo

Akiongea kwenye mkutano huo kiongozi wa jopo hilo la wachoraji, Robert Ntilo, alisema, “Huu ni mradi wawa kipekee wa Meya Silaa na tunajivunia kualikwa kushiriki na kutumia vipaji vyetu, tunaweza kuleta tofauti.”

IMG_9089
Robert Ntilo

Wasanii watakaoshiriki kuchora ni pamoja na Robino Ntila, Aggrey Mwasha, Salum Kambi, Cuthbert Semgoja, James Haule, Haji Chilonga,Thobias Minzi, Moses Luhanga, Poni Yengi Miss na Vita Malulu.

IMG_9094
Miongoni mwa wachoraji 10 watakaochora picha zitakazopigwa mnada November 16

Kampeni ya mwaka huu imepewa jina la ‘Dawati ni Elimu’ ikiwa na msemo ‘Kalisha mmoja, boresha Elimu’.

IMG_9100
Dhruv Jog wa Advent Construction Ltd

Katika kampeni mwaka huu matembezi ya hisani yalifanyika October 12 kuanzia Mnazi Mmoja hadi shule ya msingi ya Bunge na yaliongozwa na Mama Salma Kikwete ili kukuza uelewa juu ya kampeni hiyo yenye lengo la kukusanya shilingi bilioni 4.98.

IMG_9111

Fedha hizo zitatumika kununua madawati 30,487 kwaajili ya shule za manispaa ya Ilala.

.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents