MichezoUncategorized
Pombe za bure za nywika kwa mamia ya mashabiki wa Croatia, ofa ya Mario Mandzukic (+Picha)
Straika wa Croatia, Mario Mandzukic ametumia jumla ya pauni 3,000 kuwanunulia pombe mashabiki wa timu hiyo ambayo ipo kwenye michuano ya kombe la dunia.
Mandzukic alitumia kiasi hicho cha fedha kuwanunulia pombe mashabiki wa Croatia ambao wapo kwenye mji aliyotoka mchezaji huyo wakati wa mechi yao ya robo fainali dhidi ya Urusi na kushinda kwa mikwaju ya penati.
Kwa mujibu wa chombo cha Croatia news site 24Sata kimesema kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 32 anayekipiga kwenye klabu ya Juventus amewalipia zaidi ya maelfu ya mashabiki pombe kushudia mchezo huo kupitia Tv kubwa inayopatikana Brod Fortress.