Michezo
Roger Feder atakuwa nje kwa mwezi baada ya majeraha
Roger Federer ambaye ni mchezaji bora namba tatu wa Dunia katika mchezo wa Tenisi atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa mwezi baada ya kuumia goti.
Federer ambaye ana miaka 34 ni mshindi mara 17 wa Grand Slam aliumia wakati wa mashindano ya wazi ya Australian huku akiondoshwa katika hatua ya nusu fainali na Novak Djokovic wiki iliyopita.