MichezoUncategorized
Simba hawanipi presha waende tu uwanjani – Kocha mpya wa Yanga
Siku moja tu tangu kutua nchini kumalizana na Yanga kocha, Mwinyi Zahera amesema kuwa hana wasiwasi na mchezo ujao dhidi ya hasimu wao Simba SC utakao pigwa Aprili 29 uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Kupitia chombo cha habari cha MCL, Mwinyi Zahera amesema kuwa anauzoefu mkubwa wakucheza mechi za nguvu nahivyo kuwataka Simba SC waende tu uwanjani hiyo Aprili 29.
Zahera ambaye alikuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya DR Congo ametua nchini juzi usiku na tayari amekwenda Morogoro kujiunga na kikosi cha mabingwa hao watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara ambacho kimeweka kambi yake mkoani humo.