Michezo

Simba na Yanga sio uadui, mwanangu mwenyewe wa kumzaa ni Yanga – Haji Manara

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Simba, Haji Manara, amefunguka kuhusu matusi anayoyapata kutoka kwa mashabiki wa Yanga.

Akiongea kwenye kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM, Manara amesema anatukanwa sana na mashabiki wa Yanga mpaka imefikia hatua wanamuunganisha kwenye magroup yao ya Whatsapp ya timu yao.

“Ninatukanwa sana, matusi mabaya ya ushamba, na wengine wananiunga hadi kwenye magroup ya whatsapp ya Yanga,” amesema Manara.

“Simba na Yanga sio uadui ni watani wa jadi. Mimi mwanangu mwenyewe wa kumzaa ni Yanga,” ameongeza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents