Michezo

Singida United yaaga mashindano ya SportPesa Super Cup

Klabu ya Singida United imeyaaga mashindano ya SportPesa Super Cup baada ya kuktolewa na timu ya AFC Leopard ‘Ingwe’ kutoka nchini Kenya kwa hatua ya mikwaju ya Penati 5-4 kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 90, katika mchezo wa kwanza wa michuano hiyo.

Wachezaji wa klabu ya Singida United

Singida United iliyopanda ligi kuu msimu huu ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 20 kupitia kwa Mzimbabwe Kutinyu Tafadzwa, kabla ya ‘Ingwe’ hawa wa Kenya kusawazisha kupitia kwa mchezaji wao Vincent Oburu.

Wachezaji wa klabu ya Singida United wakicheza na  AFC Leopard katika mchezo wa kombe la SportPesa Super Cup

Baada ya kusawazisha timu zilicheza kwa kushambuliana kila moja kwa zamu na kosa kosa za hapa na pale hadi mchezio kuamuliwa kwa mikwaju ya penalti.

Wachezaji wa klabu ya Singida United wakicheza na  AFC Leopard katika mchezo wa kombe la SportPesa Super Cup

BY HAMZA  FUMO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents