Stars wa Harambee na Taifa kuzichapa
Timu ya Taifa ya Kenya,Harambee Stars inatarajia kuingia nchini Jumapili jioni kushuka dimbani kwa mechi ya kirafiki kati ya timu ya Taifa ya Tanzania, Kilimanjaro Stars,
siku ya Jumatatu ijayo katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, ikiwa ni kupimana nguvu kabla ya kuingia katika msahindano ya Tusker CECAFA yanayotarajiwa kuanza mapema Desemba mwishoni mw mwaka huu.
Bw. Sunday Kayuni, katibu wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania,TFF, alisema, ‘Timu ya Harambe Star inatarajia kuwasili nchini Tanzania Jumapili jioni wakijiandaa kwa mchezo huo wa kirafiki utakaochezwa jumatatu.
Kayuni aliongeza kwa kusema kuwa huo ni mchezo wa kirafiki na unafuata taratibu za shirikisho la mpira wa miguu FIFA na kuongeza kuwa kwa kufanya hivyo itawaandalia mazingira mazuri ya kujua uwezo wao uko wapi.
Aidha Kayuni alimalizia kwa kusema kuwa ilishindikana kupata timu ya kucheza na Kilimanjaro Stars kupimana uwezo hivyo kuamua kuichukua Harambe Stars kucheza nao mpira wa kirafiki ili kupata mazoezi zaidi kujiandaa katika mtanange uliopo mbele yao.