Afya

Takwimu za maambukizi ya Corona duniani yaongezeka kwa kiasi kikubwa, Taifa la Marekani laongoza kwa maambukizi Italia yaongoza kwa vifo – Video

Takwimu za maambukizi ya Corona duniani yaongezeka kwa kiasi kikubwa, Taifa la Marekani laongoza kwa maambukizi Italia yaongoza kwa vifo - Video

Kila siku kukicha maambuki ya virusi vya Corona vinaendelea kuongezeka kwa kiasi kikubwa sana kote duniani kwani mpaka siku ya leo march 30 2020, kesi zikiwa ni 723,700 huku vifo vya watu waliopoteza maisha kutokana na janga hili duniani kote vikiwa ni 34,018 na walipona wakiwa ni 152,032.

Mpaka hivi sasa taifa la Marekani ndio linaoongoza kwa maambukizi ya virusi vya Corona ingawa virusi hivi vilianzia nchini China na baadaye vikaathiri sana taifa la Italia Marekani wakiwa na kesi za corona 142,537 vifo vikiwa ni 2,510 na walipona wakiwa ni 4,767.

Taifa la Italia ndio linaoongoza kwa kuwa na watu wengi waliopoteza maisha kutokana na janga hili la Corona mpaka hivi sasa likiwa na idadi kubwa zaidi ya vifo lakini likiwa taifa la pili kwa kuwa na kesi nyingi za Corona, Italia ina kesi 97,689 vifo vikiwa ni 10,779 na waliopona wakiwa ni 13,030.

Taifa la China likiwa ni taifa ambalo kesi za maambukizi ya Corona yamepungua kwa kiasi kikubwa sana na hadi hivi sasa katika baadhi ya maeneo tayari watu wameanza kuruhusiwa kwenda kwenye shughuli zao, Kesi za Corona zikiwa ni 81,470 vifo vikiwa ni 3,304 na waliopona wakiwa ni 75,770, huku Hispania likiwa taifa la nne kwa maambukizi likiwa na kesi 80,100 vifo 6,803 na walipona wakiwa ni 14,709.

https://www.instagram.com/p/B-WWusbj3wA/

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents