Michezo

Tetesi za soka barani Ulaya Ijumaa hii, Mkurugenzi wa Juventus atua katika ofisi za United kwaajili ya Pogba, Lukaku kutua Inter kwa mkataba mnono

Mkurugenzi wa michezo wa Juventus, Fabio Paratici amesafiri kuelekea katika ofisi za Manchester United mjini London kwa ajili ya mazungumzo ya ana kwa ana juu ya uhamisho wa kiungo wa kati wa Ufaransa, Paul Pogba, mwenye umri wa miaka 26. (Sky Sports Italy via Sky Sports).Mkurugenzi wa Juventus Fabio Paratici amesafiri hadi mjini London kwa ajili ya mazungumzo ya ana kwa ana juu ya uhamisho wa kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogb

Mkurugenzi wa Juventus Fabio Paratici amesafiri hadi mjini London kwa ajili ya mazungumzo ya ana kwa ana juu ya uhamisho wa kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba

Mshambuliaji wa Manchester United na Ubelgiji Romelu Lukaku, mwenye umri wa miaka 26, amekubali mkataba wa kibinafsi na Inter Milan katika mkataba unaoweza kumlipa nyota huyo pauni milioni 6.6 za mafao hadi mwaka 2024. (Gazzetta dello Sport via Metro)

kiungo wa kati-kulia wa Crystal Palace Muingereza Aaron Wan-Bissaka, mwenye umri wa miaka 21, anapendelea kuhamia Manchester United msimu huu. Palace wanamthamanisha mchezaji huyo wa safu ya ulinzi kwa kiwango cha pauni milioni 70 . (Sky Sports)Manchester City wamekuwa wakisita kukubali thamani pauni milioni 90 ya mchezaji wa safu ya kati-nyuma Harry Maguire

Manchester City wamekuwa wakisita kukubali thamani pauni milioni 90 ya mchezaji wa safu ya kati-nyuma Harry Maguire

Manchester City wamekuwa wakikataa kukubali thamani pauni milioni 90 ya mchezaji wa safu ya kati-nyuma Harry Maguire, mwenye umri wa miaka 26 iliyowekwa na Leicester na kusema kuwa pendekezo la uhamisho wake limesitishwa kwa muda. (Daily Mail)

Meneja wa Barcelona Ernesto Valverde atamruhusu kiungo wa kati wa timu hiyo Mcroatia Ivan Rakitic, mwenye umri wa miaka 31, aondoke kwenye klabu hiyo kama timu atapata timu inayomfaa ya kumchukua . (Cadena SER – in Spanish)

Arsenal wanakamilisha mkataba kwa ajili ya mlindalango Mjerumani Markus Schubert, mwenye umri wa miaka 21, kutoka klabu ya Dynamo Dresden. (Independent)

Kiungo wa safu nyuma wa Manchester City -Kyle Walker,mwenye umri wa miaka 29, amekamilisha taratibu za kusaini mkataba mpya baada ya kurejesha mahusino mazuri na meneja Pep Guardiola. (Mirror)

Romelu Lukaku, amekubali mkataba wa kibinafsi na Inter Milan katika mkataba unaoweza kumlipa nyota huyo pauni milioni 6.6 za mafao
 Romelu Lukaku, amekubali mkataba wa kibinafsi na Inter Milan katika mkataba unaoweza kumlipa nyota huyo pauni milioni 6.6 za mafao

Borussia Dortmund wanamfuatilia kwa karibu mlinzi wa Arsenal defender Laurent Koscielny, mwenye umri wa miaka 33, ambaye anaweza kuruhusiwa kuondoka msimu huu . (Daily Mail)

Everton na Paris Saint-Germain wamo katika harakati za kumsaka mshambuliaji David Neres raia wa Brazil mwenye umri wa miaka 22 anayechezea klabu ya Ajax. (Esporte – Spanish)

Winga wa Bournemouth -Ryan Fraser, mwenye umri wa miaka 25, amedokeza kuwa ataendelea kubaki katika klabu hiyo kwa mwaka mwingine zaidi licha ya kwamba anngependa kuchezea Arsenal. (mirror)

kiungo wa kati wa Paris Saint-Germain Adrien Rabiot, mwenye umri wa miaka 24, canaweza kuendelea kuwa katika klabu hiyo licha ya kuwekwa benchi kwa kipindi karibu chote cha pili cha msimu uliopita. (ESPN)City -Kyle Walker, amekamilisha taratibu za kusaini mkataba mpya baada ya kurejesha mahusino mazuri na meneja Pep Guardiola

City -Kyle Walker, amekamilisha taratibu za kusaini mkataba mpya baada ya kurejesha mahusino mazuri na meneja Pep Guardiola

Eden Hazard mwenye umri wa miaka 28, ambaye amesaini mkataba mpya na Real Madrid , amefichua kuwa mlindalango wa zamani wa Chelsea Thibaut Courtois alisaidia kumshawishi ajiunge na Real Madrid. (Football.London)

Kiungo wa kati wa Fulham Cody Drameh, mwenye umri wa miaka 17, anatarajiwa kuwa nyota wa hivi karibuni ikuhamia Bundesliga kufuatia mkataba mpya na Eintracht Frankfurt. (Mirror)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents