Michezo
TFF ”Ni mapema kusema tumefuta Msimu”, Virusi vya Corona vyaushikilia Ubingwa wa Simba
Shirikisho la Mpira wa miguu nchini TFF, limesema kuwa endapo janga la Corona litaendelea basi msimu wa ligi utategemea maamuzi yatakayofanywa na vyombo vinavyosimamia na kuendesha ligi pamoja na Kamati ya Utendaji ya shirikisho hilo, huku ikikiri kuwa bado ni mapema kusema wamefuta msimu.
Wakati ligi hiyo ikiwa imesimama kwa muda pamoja na nyingine duniani ili kuepusha kusambaa kwa virusi vya ugonjwa wa Corona, Simba SC ilikuwa inapewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa huo kutokana na ubora wa kikosi chake na umbali wa pointi uliopo kati ya Mabingwa hao watetezi wa ligi kuu dhidi ya wanaomfuatia Azam FC na Yanga SC.