TFF yamfungia Juma Nyoso kucheza soka kwa miaka miwili
Kamati ya uendeshaji ya ligi kuu Tanzania Bara iliyokutana September 29 kupitia ripoti mbalimbali za michezo iliyochezwa ya ligi kuu na ligi daraja la kwanza nchini, imemfungia nahodha wa Mbeya City, Juma Nyoso kucheza mpira wa miguu kwa kipindi cha miaka miwili.
Pia imempiga faini ya shilingi milioni mbili kuafutia kitendo cha udhalilishaji alichomfanyia mchezaji wa Azam FC, John Bocco.
Beki huyo wa Mbeya City alirudia tena kitendo hicho cha kuwadhalilisha wachezaji wenzake wake uwanjani kiasi ambacho TFF imeahidi kumchukulia hatua kali zaidi awamu hii.
“Udhalilishaji uliofanywa leo na mchezaji mmoja wa timu ya ligi kuu tumeuona,hatua kali zitachukuliwa muda sio mrefu,tuwe na subira,” Rais wa TFF, Jamal Malinzi aliandika kwenye Twitter.
Udhalilishaji uliofanywa leo na mchezaji mmoja wa timu ya ligi kuu tumeuona,hatua kali zitachukuliwa muda sio mrefu,tuwe na subira.
— Jamal Malinzi (@jamalmalinzi) September 27, 2015
Nyoso amewahi pia kumfanyia kitendo hicho mshambuliaji wa Simba, Elius Maguri na TFF kumwadhibu.