Burudani
Nicki Minaj kutayarisha na kuonekana kwenye tamthilia ya maisha yake
Nicki Minaj anatarajiwa kuwa mtayarishaji mkuu wa tamthilia mpya kupitia ABC Family itakayoangaza maisha ya rapper huyo alivyokulia kwenye viunga vya Queens, New York.
Mradi huo kutoka Kapital Entertainment, utatengeneza episode ya kwanza mwaka huu.
Tamthilia hiyo inaandikwa na Kate Angelo (Sex Tape), na itaangaza maisha ya Minaj aliyekulia Queens miaka ya 1990 pamoja na familia yake, alivyoanza muziki hadi kuwa maarufu.
Kabla ya kuwa staa, Minaj amewahi kusomea muziki kwenye shule ya kifahari, LaGuardia High School ya Manhattan.
Amewahi kuigiza kwenye filamu kama Ice Ace: Continental Drift kwa kuingiza sauti, filamu ya The Other Woman na hivi karibuni aliigiza kwenye filamu ya Ice Cube, Barbershop 3.