Picha
THT yatembelea watoto wanaotibiwa kansa Muhimbili
Wasanii wa nyumba ya vipaji Tanzania (THT), jana walitembelea watoto wanaopata matibabu ya kansa katika hospitali ya Taifa Muhimbili, ili kuwafariji na kuwapa moyo wa kuendelea na matibabu ya ugonjwa huo.
Ziara hiyo ambayo ilijumuisha wasanii wote wa nyumba ya vipaji kama Ditto, Mwasiti, Barnaba, Amini, Linah, Makomando, Ali Nipishe, Mataluma na The Trio, iliwapa fursa watoto kuzungumza na wanamuziki hao wanaowapenda pamoja na kupata burudani ya muziki kutoka kwao.
Watoto hao ambao wanaishi katika hosteli na familia zao, wako chini ya taasisi isiyo ya kiserikali inayoitwa Tumaini la Maisha Tanzania ikihudumia zaidi ya kaya ishirini na nne.
Wakizungumza hospitalini hapo baada ya kuwaona wagonjwa hao, msanii Ditto alisema wameamua kutoa muda wao ili kuwafariji watoto hao kama mchango wao kwa jamii.
‘Ugonjwa wa kansa ni tatizo kubwa katika jamii yetu na ndio maana sisi kama THT tumeamua kuja hapa kuonyesha tunawajali na wao ni sehemu ya jamii yetu hivyo wasijisikie wametengwa’ alisema Ditto.
Nao watoto wanaopata matibabu hospitalini hapo walipongeza wasanii wa THT kwa kuwakumbuka, huku wakiomba wasanii wengine na jamii isiwasahau.
Ziara hiyo ambayo ilijumuisha wasanii wote wa nyumba ya vipaji kama Ditto, Mwasiti, Barnaba, Amini, Linah, Makomando, Ali Nipishe, Mataluma na The Trio, iliwapa fursa watoto kuzungumza na wanamuziki hao wanaowapenda pamoja na kupata burudani ya muziki kutoka kwao.
Watoto hao ambao wanaishi katika hosteli na familia zao, wako chini ya taasisi isiyo ya kiserikali inayoitwa Tumaini la Maisha Tanzania ikihudumia zaidi ya kaya ishirini na nne.
Wakizungumza hospitalini hapo baada ya kuwaona wagonjwa hao, msanii Ditto alisema wameamua kutoa muda wao ili kuwafariji watoto hao kama mchango wao kwa jamii.
‘Ugonjwa wa kansa ni tatizo kubwa katika jamii yetu na ndio maana sisi kama THT tumeamua kuja hapa kuonyesha tunawajali na wao ni sehemu ya jamii yetu hivyo wasijisikie wametengwa’ alisema Ditto.
Nao watoto wanaopata matibabu hospitalini hapo walipongeza wasanii wa THT kwa kuwakumbuka, huku wakiomba wasanii wengine na jamii isiwasahau.