Michezo

Timu ya wasichana ya Tanzania yang’ara kombe la Dunia Urusi

Timu ya Wasichana ya Tanzania inayoundwa na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu kutoka kituo cha TSC cha jijini Mwanza wakiwa Moscow imeibuka na ushindi wa goli 1 – 0 dhidi ya Kazakhstan kwenye Kombe la Dunia la Watoto wanaoishi mazingira magumu.

Timu hiyo ya Wasichana ya Tanzania kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu mpaka sasa imeibuka na ushindi kwenye michezo miwili wakwanza dhidi ya wenyeji Urusi kwa mabao 3 – 0 na timu ya Kazakhstan goli 1 – 0 michuano ya Kombe la Dunia la Watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.

Timu ya wavulana ya Tanzania kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wakiwa na kombe hilo la ubingwa wa Dunia 2014.

Mwaka 2014 timu ya wavulana ya Tanzania kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu walitwaa kombe hilo la ubingwa wa Dunia na kupokelewa na aliyekuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda mjini Dodoma Aprili 11, 2014

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents