Burudani

Uchaguzi wa Kenya wamfanya Nyota Ndogo kushindwa kuweka wazi matatizo yake ya miaka 17

Nyota Ndogo ameshindwa kufanya kama alivyoahidi kueleza kila kitu ambacho kimekuwa kikimtesa kwa takriban miaka 17 sasa.

Sababu kubwa ambayo muimbaji huyo wa Kenya kushindwa kuweka wazi kama alivyoahidi ni kutokana na maandalizi ya uchaguzi mkuu wa Urais wa nchi hiyo ambao unaotarajiwa kufanyika hapo kesho.

Kupitia mtandao wa Instagram, Nyota Ndogo ametaja sababu hiyo kwa kuandika, “Pole nimechelewa. But pia nilikua nauliza kwa ajili ya uchaguzi unaoendelea Kenya.”

“Niipe mpaka kesho? niwape muda wa kuelekeza akili zenu kwenye uchaguzi? muhimu pia sana,” ameongeza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents