Technology

Ufahamu uwezo wa ndege mpya Boeing 787-8 Dreamliner (Picha)

Jumapili hii ilikuwa ni siku ya furaha na vifijo kwa Watanzania baada ya kushuhudia ndege mpya ya Tanzania Boeng 787-8 Dreamliner inayobeba abiria 262 ilikiwasili katika uwanja wa ndege wa JK Nyerere.

Ndege ya Boeing 787-8 Dreamliner ni ya ukubwa wa wastani, yenye injini mbili inayotengenezwa na kampuni ya Boeing ya Marekani.

Matumizi yake ya mafuta ni wa asilimia 20 chini cha ndege ya ukubwa sawa na huo na ndiyo ndege ya Boeing inayotumia kiwango cha chini zaidi cha mafuta.

Injini zake zimejengwa kwa njia maalumu ili kupunguza sauti ndani na pia nje ya ndege kwa hadi asilimia 60.

Madirisha yake ni makubwa kuliko ya ndege zingine za ukubwa kama huo kwa asilimia 30.

Ukiwa ndani ya ndege hii una uwezo wa kupunguza mwangaza wa dirisha kwenye ndege kwa kutumia teknolojia ya kabadilisha rangi ya kioo kukiwezesha kudhibiti mwanangaza unaoingia.

Ina uwezo wa kubeba hadi abiria 262 ikiwa pia na uwezo wa kusafiri umbali wa kilomita 13,621 bila kusimama.

Boeing 787-8 ilijengwa kuchukua mahala pa ndege aina za 67-200ER na 300ER.

Fahamu uwezo wake na jinsi ilivyotengenezwa.




Source: Modernairliners/BBC/Airliners.net

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents