Michezo

Ureno imetwaa ubingwa wa Ulaya, Euro 2016

Timu ya taifa ya Ureno imetwaa ubingwa michuano ya Ulaya, Euro 2016, kwa kuwafunga wenyeji Ufaransa 1-0 katika dakika za ziada kwenye mchezo wa fainali mjini Paris.

3624A8EB00000578-3683538-image-a-34_1468188365389

3624A7EF00000578-3683538-image-a-35_1468188386529

Goli la ushindi lilifungwa na Eder katika dakika ya 110, na kupeleka kilio na huzuni kwa mashabiki wa Ufaransa waliofurika kwenye uwanja wa Stade de France.

36246AC900000578-3683538-image-a-8_1468185996645

36246ACD00000578-3683538-image-a-22_1468187288452

Ilikuwa furaha kubwa kwa mashabiki wa Ureno. Hii ni mara ya kwanza Ureno kushinda michuano mikubwa.
Ureno walicheza kwa kujituma na ushirikiano bila ya mchezaji wao nyota Cristiano Ronaldo aliyetoka kutokana na kupata jeraha la goti katika kipindi cha kwanza.

Ufaransa ilitawala mchezo kwa kiasi kikubwa, lakini hawakuweza kuzitumia vyema nafasi walizopata.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents