Vanessa Mdee ashoot video ya ‘Closer’ juu ya jengo la ghorofa 17 jijini Nairobi
Vanessa Mdee sio shabiki wa vitu rahisi rahisi! Mtangazaji huyo na muimbaji wa Closer amekamilisha kushoot video ya wimbo wake huo jijini Nairobi. Sio video ya kawaida kwasababu nyingi.
Sababu ya kwanza ni director wa video hiyo, Andrew Macharia ambaye ameshawahi kutengeneza nyimbo za wasanii wakubwa duniani akiwemo Young Jeezy. Andy mwenye umri wa miaka 23 ndiye aliyeiongoza video ya wimbo wa Camp Mulla ‘Fresh All Day’.
Sababu ya pili ni location ya video hiyo ambapo katika miongoni mwa scenes zake, Vanessa ataonekana juu ya jengo lenye ghorofa 17.
“When your director will have you dancing atop a 17 story building to get that money shot – you’re either disposable or a flame,” aliandika Vanessa kwenye picha aliyoiweka Instagram.
Bila wasiwasi video ya Closer itakuwa kali. Hongera kwa timu inayomsimamia.