Michezo
Video: Timu ya Clouds yaibuka na ushindi dhidi ya Wasanii wakiongozwa na Roma, Godzilla pamoja na Wakazi
Kuelekea tamasha kubwa la muziki nchini linalotarajiwa kufanyika hii leo Novemba 24 mwaka 2108, hapo jana usiku timu ya Clouds Media ilicheza mchezo wa kirafiki wa Basketball maarufu kama mpira wa kikapu dhidi ya Wasanii wa bongoflave waliyoongozwa na Roma,Godzilla pamoja na Wakazi.
Katika mchezo huo uliyokuwa na ushindani mkubwa ulianza majira ya saa 11 jioni katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es salaam na kumalizika usiku ilishuhudia timu ya Clouds Media ikifanikiwa kuibuka na ushindi wa jumla ya vikapu 66 dhidi ya 63 walivyopata wasanii.
https://www.instagram.com/p/BqjW6O8B0KP/