Video/Picha: Flaviana Matata azindua stationery zake kwa kutoa msaada kwenye shule ya msingi Minazini, Dar
Mwanamitindo wa kimataifa, Flaviana Matata, leo amezindua stationery zake zilizopo chini ya taasisi ya Flaviana Matata Foundation.
Uzinduzi huo umefanyika kwenye shule ya msingi Minazini, iliyopo Mwananyamala B, jijini Dar es Salaam ambapo pia ametoa msaada wa vifaa mbalimbali vya shule vyenye brand yake ya Flaviana Matata Foundation yakiwemo madaftari, kalamu za kuandikia na vifaa vingine vya shuleni.
Miongoni mwa watu waliohudhuria uzinduzi huo ni pamoja na Nancy Sumari na msanii wa Tupogo, Ommy Dimpoz
Akiongea na Bongo5 kwenye uzinduzi huo, Flaviana amesema amefanya uzinduzi kwa kutoa msaada huo kwakuwa lengo la taasisi yake ni kusaidia wanafunzi wasio na uwezo.
“Hapa shuleni kuna wanafunzi hawajiwezi, tukasema tuje tuzindue stationery, tuconnect na wanafunzi, waone kile tunachokifanya, tusikilize pia matatizo yao,” alisema Flaviana ambaye alizitaja stationery zitakazokuwa zikizalishwa chini ya taasisi yake kuwa ni pamoja na madaftari, kalamu za wino, penseli, ufuto, rula na compass.
Flaviana akionesha daftari na kalamu zake
Aliongeza kuwa pamoja na kwamba vifaa hivyo vya shule vitakuwa vikiuzwa, kuna watu watakaokuwa wakipewa msaada.
Pia amezikaribisha taasisi na makampuni nchini kununua vifaa hivyo na kisha kutoa misaada kwenye shule mbalimbali nchini.
Faraja Kotta
Flaviana akisaini kitabu cha wageni
Flaviana Matata akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Minazini
Flaviana Matata na Myler Nyangasa wakiwa wameshikilia
Marafiki wa karibu wa Flaviana akiwemo Khadija Mwanamboka, kushoto
Myler Nyangasa, Flaviana na Elligiver
Nancy Sumari na Faraja Kotta wakiziangalia stationery za FMF
Ommy Dimpoz, kushoto alijitokeza kumuunga mkono Flaviana kwenye uzinduzi huo