Michezo

Viwanja 12 kuanza kutimua vumbi kombe la Dunia leo nchini Urusi

Michuano ya kombe la Dunia kwa mwaka huu 2018 inatarajia kuanza kutimua vumbi hii leo Juni 14 nchini Urusi huku mwenyeji akikabiliana na Saudi Arabia mchezo wa ufunguzi utakao pigwa dimba la Luzhniki jijini Moscow.

Kwenye michuano hiyo wapenzi wa mchezo wa soka watashuhudia jumla ya timu 32 zikishuka dimbani kucheza michezo 64 ambayo itapigwa kwenye viwanja 12 vinavyopatikana kwenye miji 11 ya nchini Urusi ndani ya siku 32.

Mabingwa wa kombe hilo wa mwaka 1966 timu ya taifa ya Uingereza wataanza michuano hiyo Jumi 18 kwa kuwakabili Tunisia.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents