Michezo
Wachezaji wa Simba wapimwa afya Afrika Kusini (Video)
Baada ya hivi karibuni Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kutoa kanuni mpya zinazohitaji klabu zote zinazoshiriki ligi inayosimamiwa na shirikisho hilo kuhakikisha wanawafanyia vipimo vya afya wachezaji wake, mabingwa wa FA Simba SC imeanza zoezi hilo kwa wachezaji wake watakao tumiwa katika mashindano mbali mbali.
Miongoni mwa wachezaji wa kikosi cha Simba waliofanyiwa vipimo hivyo ni pamoja na Laudit Mavugo beki, Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ wakifanyiwa vipimo vya afya tayari kwa msimu ujao, vipimo hivyo vimefanyika nchini Afrika Kusini chini ya usimamizi wa daktari wa timu hiyo Dk. Yassin Gembe.
Wachezaji wasiopimwa afya marufuku viwanjani – TFF
By Hamza Fumo