MichezoUncategorized
Wenger athibitisha David Ospina kuanza dhidi ya Man City
Meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema mlindalango wake, David Ospina ataanza katika mchezo wao wa siku ya Jumapili wa michuano ya EFL dhidi ya Manchester City.
Mchezaji Aaron Ramsey atakuwa sehemu ya mchezo huo utakao pigwa katika dimba la Wembley huku Mesut Ozil akitarajiwa kurejea baada ya kusumbuliwa na majeraha ya kifundo cha mguu.
Wenger amethibitisha hilo huku akisema Alexandre Lacazette anaendelea vema na baada ya kupata majeraha na anatarajiwa kurejea baada ya wiki nne waka Ramsey akiwa chini ya uangalizi kabla ya kuruhusiwa kuwa sehemu ya mchezo huo wa Jumapili.